Acts 2:1-4

Kushuka Kwa Roho Mtakatifu

1 aSiku ya Pentekoste ilipowadia, waamini wote walikuwa mahali pamoja. 2 bGhafula sauti kama mvumo mkubwa wa upepo mkali uliotoka mbinguni ukaijaza nyumba yote walimokuwa wameketi. 3 cZikatokea ndimi kama za moto zilizogawanyika na kukaa juu ya kila mmoja wao. 4 dWote wakajazwa na Roho Mtakatifu, wakaanza kunena kwa lugha nyingine, kama Roho alivyowajalia.

Copyright information for SwhNEN